Search your Topic here

Friday, August 7, 2015

CHAKULA DAWA KUONDOA TATIZO LA MBEGU ZA KIUME


Ili kutatua tatizo ni muhimu kung’oa kabisa
mzizi wake. Mwili wako una maarifa ya
kujirekebisha pasipo kuhitaji vilevi au
mawada, unachotakiwa kuzingatia ni chakula
bora tu. Wahenga walisema, utakuwa bora
kama chakula unachokula. Je wewe unakula
chakula bora ili kulinda heshima yako
nyumbani?
Vitu vinavyoweza kupelekea kupungua kwa
nguvu za kiume ni kama:
Kutokuwa na mzunguko mzuri wa
damu mwilini, hasa sehemu za viungo
vya uzazi kwa mwanaume.
Kutokuwa na kiwango cha kutosha cha
homoni ya Testosterone
Kupungukiwa protini na hivyo kukosa
amino asidi mwilini
Jinsi ya kuongeza nguvu za
kiume
Leo napenda tuangalie vyakula ambavyo
vinasaidia kuboresha nguvu za kiume na
kusaidia kwa kiasi kikubwa kudumisha
mapenzi na kulinda mahusiano na ndoa.

1. Blueberry 

Blueberry ni matunda yanayosaidia sana
kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea
kuyaita ‘viagra’ asilia kutokana na kazi
inayoifanya mwilini. Blueberries ina
virutubishi vinavyoimarisha mishipa ya damu
na kusaidia mzunguko mzuri wa damu
mwilini. Damu ndio kila kitu katika nguvu za
kiume. Vilevile, blueberries zina nyuzinyuzi
( fiber ) ambazo husaidia kuondoa kolesteroli
(Cholestrol) mwilini kabla hazijanganda
kwenye mishipa ya damu. Kuwa na mzunguko
mzuri wa damu husaidia mwanaume aweze
kuhimiri mapenzi wa muda mrefu zaidi.
Soma pia : Njia 7 za kuongeza uzito

2. Mtini(figs)

Mtini (figs) ni matunda yenye kiwango
kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo
kikubwa katika kuzalisha homoni mwilini.
Homoni ndio kishawishi cha nguvu za kiume
mwilini. Kukosa amino asidi huweza
kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au
kupungukiwa na nguvu za kiume.
3. Chaza/Kombe wabichi (Raw Oysters)
Chaza wana kiwango kikubwa cha madini ya
zinc. Madini za zinc hutumika katika
utengenezaji wa homoni ya testosterone,
shahawa na mbegu za kiume . Uwingi wa
uzalishwaji wa testosterone mwilini huathiri
pia hamu ya mapenzi na nguvu za kiume –
ikiwa kidogo huondoa hamu, ikiwa nyingi
hupelekea hamu na nguvu zaidi.
Kupungukiwa kwa madini ya zinc
husababisha kupungua kwa nguvu za kiume,
udhaifu (uhanithi), na kushuka kwa kiwango
cha uwezo wa kufanya mapenzi.

4. Karanga 

Karanga ni chanzo kikubwa cha kujenga
protini mwilini. Karanga huwa na kiwango
kikubwa cha amino asidi ambayo husaidia
kuweka vizuri mfumo wa damu, hivyo
kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha
ufanyaji mapenzi.

5. Vitunguu saumu 

Kitunguu saumu kina allicin, kiambato
kinachosaidia mzunguko mzuri wa damu
kwenye viungo vya uzazi. Kuwa na mzunguko
mzuri wa damu kwenye uume ni sababu
kubwa ya kuongeza stamina ya kufanya
mapenzi.
Soma pia: Jinsi afya ilivyo muhimu kwako

6. Ndizi

Kuwa na stamina ni muhimu katika ufanyaji
mapenzi. Ndizi ni chanzo kikubwa cha
vitamin B ambayo husaidia sana katika
kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa
wakati wa kufanya kazi nzito. Ndizi ina
kimeng’enyo cha Bromelain ambacho
huongeza nguvu za kiume, ashki ya mapenzi
( libido).

7. Chocolate
Chocolate inasaidia kuongeza stamina
kwenye kufanya mapenzi kwasababu ina
viambato vya phenylethylamine na alkaloid .
Phenylethylamine ni kiambato
kinachopelekea kujisikia vizuri, hasa wakati
wa kufanya mapenzi na alkaloid huongeza
stamina na nguvu wakati wa mapenzi.

Tumia vyakula asili Zaidi ILI kuboresha Afya yako

No comments:

Follow us