Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema haya jijini Mbeya, wakati akizinduzi dula la MSD pamoja na Ghala la kisasa la kuhifadhia dawa, ambalo litahudumia mikoa ya nyanda za juu kusini, huku akidai kuwa uanzishwaji wa maduka hayo haukusudii kuuwa maduka ya dawa ya watu binafsi, isipokuwa yatajifunga yenyewe kwa kuwepo kwa dawa zote kwenye maduka hayo, nakwamba wafanyabiashara hao wanatakiwa kufanya biashara nyingine na si zinazogusa maisha ya watu.
Aidha Waziri huyu amesema wapo baadhi ya watumishi wa afya ambao siyo waaminifu wanaihujumu serikali kwa kuuza dawa, ambapo ameiagiza serikali ya mkoa kufanya msako ili kubaini maduka ya watu binafsi yanayouza dawa za serikali na kuwachukulia hatua.
No comments:
Post a Comment